Tuesday, December 1, 2015

WASWAHILI WANASEMA MAJI HUFUATA MKONDO...! KWA HAYA ANAYOYAFANYA MTOTO WA ZIDANE...!


  

Kwenye mechi hiyo Luca Zidane alitolewa nje kwenye mechi hiyo kwa kosa la kumkwatua mchezaji mwenzake, lakini pia kabla hajapewa kadi hiyo alileta ubabe wa kumvimbia mwenzake kwa kusukumana kwa kichwa kama Mbuzi wanavyofanyaga
 
                   Luca Zidane alipewa kadi nyekundu baada ya kumkwatua mchezaji wa Atletico Madrid

   Luca Zidane ambae ni goli kipa wa club ya Real Madrid kwenye kikosi cha under 17 amepewa kadi nyekundu kwenye mechi dhidi ya wapinzani wao Atletico Madrid.

             Luca Zidane (katikati) alionekana akimpiga kichwa mchezaji wa Atletico Madrid

  Dogo huyu ameingia kwenye vichwa vya habari baada ya kitendo hicho kufananishwa na baba yake ambae aliwai kumpiga kichwa Marco Matellazi kwenye fainali za Kombe la Dunia mwaka 2006

  

Zidane ana watoto wa 4 ambapo Enzo mkubwa ni captain wa Real Madrid B, Luca anacheza kwenye kikosi cha under 17 na Theo na Elyaz wanacheza kwenye Academy

No comments :