Sunday, January 10, 2016

PONGEZI ZA PEKEE KWA MBWANA SAMATTA TOKA KWA WATANZANIA NA UNAWAKUMBUSHA WATANZANIA KILE KILICHOFANYWA TAIFA STARS 1973 PALE LAGOS NIGERIA TOKA KWA Maulid Dilunga PAMOJA NA Omar Mahadhi

Mbwana Samatta alipokelewa na familia yake, watanzania kijumla alipowasili jana saa 8 usiku Uwanja wa ndege wa JKN jijini Dar es 
Salaam
Ni miaka 42 imepita tangu Tanzania ing’are katika medani ya soka Afrika.

MSHAMBULIAJI Maulid Dilunga wa Yanga na kipa Omar Mahadhi wa Simba ni wachezaji pekee wa Tanzania walioweka historia ya kuteuliwa kuunda kikosi cha Afrika.
Uteuzi huo ulifanywa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF), mara baada ya kumalizika kwa michezo ya All Africa Games, iliyofanyika mwaka 1973 mjini Lagos, Nigeria.
Katika michezo hiyo, Taifa Stars ilifanikiwa kufika hatua ya nusu fainali. Katika mechi za awali, Stars ilitoka suluhu na Nigeria A, ikaichapa Nigeria B mabao 2-1 kabla ya kuzifunga Ghana na Togo bao 1-0 kila moja.
Katika hatua iliyofuata, Stars ilitoka suluhu na Nigeria, ikatoka sare ya bao 1-1 na Misri kabla ya kufungwa mabao 2-1 na Algeria.
Dilunga ndiye aliyeibuka mchezaji nyota wa Taifa Stars katika michezo hiyo baada ya kuifungia mabao yote katika kila mechi.
Licha ya Stars kutolewa hatua ya nusu fainali, Dilunga na Mahadhi hawawezi kuisahau michezo hiyo kutokana na kuteuliwa kwenye kikosi cha kombani ya Afrika.
Mara baada ya uteuzi huo, kikosi hicho kilifanya ziara katika mataifa sita ya Ulaya na Amerika, ambako kilicheza mechi kadhaa za kirafiki.
Baadhi ya mataifa hayo ni Mexico, Guatemala, Uruguay, Peru, Hungary na Bulgaria. Katika ziara hiyo, kikosi hicho cha Afrika kilishinda mechi tatu, kilitoka sare mbili na kufungwa moja.
Uteuzi wa Dilunga kwenye kikosi hicho uliingia utata baada ya kilichokuwa Chama cha Soka nchini (FAT) wakati huo, kudhani mchezaji aliyeteuliwa ni Abdalla Kibadeni.
Katika taarifa yake kwa FAT, CAF ilisema inamhitaji mchezaji aliyekuwa akivaa jezi namba 10. Na katika kikosi cha Stars wakati huo, wachezaji waliokuwa wakivaa jezi hiyo ni Dilunga na Kibadeni.
Ikabidi FAT iombe ufafanuzi kwa CAF na ndipo ilipobainika kwamba, mchezaji aliyekuwa akihitajika ni Dilunga na siyo Kibadeni.
Kilichoivutia CAF kumteua Dilunga kwenye kikosi hicho ni uwezo wake mkubwa wa kufunga mabao, hasa katika mechi yao dhidi ya Nigeria B, ambapo alipachika wavuni mabao mawili.
Dilunga pia aliwahi kupata nafasi ya kwenda kucheza soka ya kulipwa Ulaya mwaka 1970 wakati timu ya daraja la pili ya West Bromwich ya England ilipofanya ziara nchini.
Hata hivyo, kuna madai kuwa, aliyekuwa mwenyekiti wa FAT wakati huo, Saidi Hamad El-Maamry alimzuia kwenda huko ili aweze kuichezea Taifa Stars katika michuano ya kimataifa.
Viongozi wa West Bromwich walikuja nchini wakiwa wageni wa Yanga na baada ya kucheza mechi moja ya kirafiki, walivutiwa na uwezo wa Dilunga.
Mbali na kuzuiwa na El-Maamry kwenda Uingereza, mwamko mdogo kwa wanasoka wa Tanzania kwenda kucheza soka ya kulipwa nje nao ulichangia kumfanya Dilunga apuuze mwito huo
Nyota hiyo iliyoanzia kwa mshambuliaji Maulid Dilunga na kipa Omari Mahadhi, iling’ara pia juzi kwa Mbwana Samatta aliyeteuliwa katika kikosi bora cha mwaka Afrika.
Samatta aliungana kikosini na kipa Robert Kidiaba (DR Kongo), mabeki; Serge Aurier (Cote d’Ivoire), Aymen Abdennour (Tunisia), Mohamed Meftah (Algeria), viungo; Andre Ayew (Ghana), Yaya Toure (Cote d’Ivoire), Sadio Mane (Senegal), Yacine Brahim (Algeria) na washambuliaji; Pierre-Emerrick Aubameyang (Gabon) na Baghdad Bounedjah (Algeria).
Samatta, amebebwa na mafanikio makubwa katika soka akiwa na klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), yakiwamo ya kuwa mfungaji bora wa Ligi ya Mabingwa Afrika akiwa na mabao saba.
Hayo ni mafanikio makubwa yanayorejesha kumbukumbu za kina Dilunga na Mahadhi (wote sasa ni marehemu), walioteuliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kuunda kikosi cha nyota Afrika, Africa All Stars, mwaka 1973.
Tofauti na Samatta aliyeibuka mshindi wa tuzo ya mchezaji bora Afrika mwaka 2015 kwa wanaocheza soka ndani Afrika akiwa na TP Mazembe, Klabu Bingwa ya Afrika, Dilunga na Mahadhi walitokea Yanga na Simba na kikosi cha Taifa Stars kilichoshiriki michezo ya Afrika mwaka 1973 mjini Lagos, Nigeria.
Taifa Stars , wakati ule ilicheza nusu fainali baada ya kufanya vyema kwenye michezo ya awali kwa kuibana Super Eagles au Nigeria A na kutoka 0-0, ikaichapa Nigeria B kwa mabao 2-1, yaliyofungwa na Dilunga.
Pia, timu hiyo ilizifunga timu zinazotamba leo Afrika, Ghana na Togo, bao 1-0 kila moja na baada ya mashindano hayo, CAF iliwateua wachezaji hao kuiwakilisha Afrika, ambako walizuru Hungary, Bulgaria barani Ulaya pia kutembelea Mexico, Guatemala, Uruguay, Peru. Rekodi zinaonyesha kuwa kikosi hicho cha kina Dilunga, Mahadhi kilishinda mechi tatu, sare mbili na kufungwa mechi moja.
Hata hivyo, uteuzi wa Dilunga kwenye kikosi hicho ulizua utata baada ya kilichokuwa Chama cha Soka nchini (FAT, sasa TFF), kudhani mchezaji aliyeteuliwa alikuwa Abdallah Kibaden.
Majibu ya CAF kwa FAT, yalieleza kuwa shirikisho hilo lilimhitaji mchezaji aliyekuwa akivaa jezi namba 10 Stars, ambayo wakati ule ilivaliwa nao, Dilunga na Kibaden.
FAT ililazimika kuomba ufafanuzi CAF na ndipo ilipobainika kwamba, mchezaji aliyehitajika ni Dilunga na siyo Kibaden.
Sababu za CAF kumteua Dilunga ni uwezo wake mkubwa wa kufunga mabao, aliouonyesha kwenye mechi dhidi ya Nigeria B, ambako alipachika wavuni mabao mawili akitokea benchi.
Dilunga, aliyetokea Shule ya Sekondari Mzumbe, Morogoro kabla ya kutua Yanga mwaka 1966, pia aliwahi kupata nafasi ya kucheza soka la kulipwa England mwaka 1970 kwenye timu iliyokuwa Daraja la Pili , West Bromwich, ambayo kwa sasa ipo Ligi Kuu.
Timu ilizuru Tanzania kucheza na Yanga na hadi leo kuna madai kuwa aliyekuwa mwenyekiti wa FAT, Said Hamad El-Maamry alimzuia Dilunga kwenda Ulaya ili aichezee Taifa Stars michezo ya kimataifa.
Alipoulizwa jana kuhusu mzozo huo wa Dilunga na Kibaden, El- Maamry alijibu kuwa hawezi kulizungumzia, badala yake waulizwe viongozi wa FA ndio wasimamizi wa soka nchini.

No comments :